MECHI
ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kati ya wenyeji Yanga na Mbeya
City iliyofanyika jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh.
175,285,000.
Watazamaji 30,411 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo kwa viingilio sh. 5,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 kwa VIP A. Yanga ndiyo iliyoibuka na ushindi wa bao 1-0.
Watazamaji 30,411 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo kwa viingilio sh. 5,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 kwa VIP A. Yanga ndiyo iliyoibuka na ushindi wa bao 1-0.
Mgawanyo
wa mapato ulikuwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 26,738,389.83,
gharama za kuchapa tiketi sh. 2,919,200 wakati kila klabu ilipata sh.
42,960,086.50.
Uwanja sh. 21,844,111.53, gharama za mechi sh. 13,106,466.92, Bodi ya Ligi sh. 13,106,466.92, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 6,553,233.46 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 5,096,959.36.
Uwanja sh. 21,844,111.53, gharama za mechi sh. 13,106,466.92, Bodi ya Ligi sh. 13,106,466.92, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 6,553,233.46 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 5,096,959.36.
Nayo
mechi ya Simba na Oljoro JKT iliyochezwa Februari 1 mwaka huu kwenye
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 47,705,000 ambapo kila timu
imepata sh. 11,254,122 kutokana na watazamaji 8,267.
Mgawanyo
mwingine katika mechi hiyo iliyomalizika kwa Simba kushinda mabao 4-0
ni Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 7,277,033.90 na gharama za
kuchapa tiketi sh. 2,278,400.
Uwanja
sh. 5,722,434.92, gharama za mechi sh. 3,433,460.95, Bodi ya Ligi sh.
3,433,460.95, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh.
1,716,730.47 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA)
sh. 1,335,234.81.
Wakati
huo huo: Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limepata hati ya kiwanja
chake kilichopo eneo la Mnyanjani katika Jiji la Tanga.
Hati hiyo ya miaka 99 ya kiwanja hicho namba 75 Block D chenye ukubwa wa ekari 7.6 ilikabidhiwa kwa TFF, Januari 13 mwaka huu.
Kiwanja hicho kitaendelezwa kwa matumizi mbalimbali, kubwa ikiwa ni uwanja wa mpira wa miguu.
Kiwanja hicho kitaendelezwa kwa matumizi mbalimbali, kubwa ikiwa ni uwanja wa mpira wa miguu.
Katika
hatua nyingine, TFF itaadhimisha miaka 50 tangu lipate uanachama wa
Shirikisho la Soka la Kimataifa (TFF) kwa shughuli mbalimbili ikiwemo
michezo na makongamano.
Kamati
maalumu itaundwa kwa ajili ya kupanga na kuratibu shughuli hiyo ambayo
TFF imepanga kuadhimisha nchini nzima kwa kutumia wanachama wake.
TFF wakati huo ikiitwa Chama cha Mpira wa Miguu Tanzania (FAT) ilijiunga na FIFA Oktoba 8, 1964.
TFF wakati huo ikiitwa Chama cha Mpira wa Miguu Tanzania (FAT) ilijiunga na FIFA Oktoba 8, 1964.
Tupe maoni yako
