banner

.

.

Monday, 3 February 2014

HOSPITALI YA KAHAMA YAKABILIWA NA UKOSEFU WA VITENDANISHI VYA CD4


Elizabeth Maxmillian
Kahama

HOSPITALI ya serikali  wilayani kahama mkoani shinyanga inakabiliwa na ukosefu wa vitendanishi vya kupimia CD 4 kwa kipindi cha miezi miwili hali hali ambayo imekuwa ikisababisha baadhi a wagonjwa kupoteza maisha kabla ya kutumia dawa za kuuwa akali ya VVU.

Hayo yameelezwa jana na mganga mkuu wa halmashauri ya mji wa kahama Dr ,Deo Nyaga baada ya madiwani  kutoa malalamiko  wanayoyapata toka kwa wananchi ambao wamekuwa wakipima na kugundulika wana maambukizi ya virusivya ukimwi.

Aidha akitoa akitoa ufafanuzi juu ya jambo hilo Dr Nyaga aliosema kuwa tatizo kubwa linaloikabili hospitali hiyo ni ukosefu wa vitendanishi ambapo kwa sasa takribani miezi miwili imepita ikiwa hakuna huduma ya upimaji wa CD4 inayoendelea  huku ikiwa  wanategemea kupata toka bohari kuu MSD.

Hata hivyo alisema kufuatia hali hiyo wameanza kuangalia utaratibu wa kuwaanzishia dawa wagonjwa ambao kinga zao zitaonekana kukubalika kukabiliana na dawa hizo wakati wakisubili uletwaji wa vitendanishi vya kupimia CD4 .

Kwa upande wao madiwa  wa halmashauri ya mji wa kahama wamemtaka mganga huyo kukaa pamoja na watumishi wengine wa afya na kuwaeleza ukweli kutumia lugha zisizo faa kwa wagonjwa hasa wa Ukimwi ambao kwanamna moja ama nyingine wanaweza kukatishwa tama na kukosa matumaini kutokana na lugha za wahudumu kutokuwa nziri.

Akitoa malalamiko hayo diwani wa kata ya mwendakulima Ntabo Majabi alisema kuwa katika utoaji wa dawa  kwa wagonjwa kuna ukiritimba unaofanywa na wahudumu wa afya katika hospitali hiyo ya wilaya wa kuwabaguwa watu wanaowafahamu na kuwapatia dawa huku wengine wasiojulikana wakibaki wamapenga mstari na kujikuta  dawa zikiwaishia .

Nae mwenyhekiti wa halahsuri ya mji wa kahama Machibya  Chidulamabambase aliwataka viongozi wa kata na vijijiji kushirikiana na wataalamu wa afya kwa kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananchi wao juu ya kutumia dawa  za kupunguza makali ya VVU kutokana na wagonjwa waliowengi kukata tama baada ya kukosekana kwa vitendanishi vya kupimia CD4.

Tupe maoni yako