banner

.

.

Saturday 1 February 2014

CHADEMA M4C PAMOJA DAIMA YAHITIMISHWA MWANZA KATIKA UWANJA WA FURAHISHAA. DR. SLAA ATOA TAMKO.

Wananchi wa Jiji la Mwanza wameinua mikono ishara ya Kusurrender katika Mkutano wa hitimisho a Chadema M4C Pamoja Daima ulifanyika katika Uwanja wa Furahisha Jijini Mwanza Jioni la Leo.
 Chopa iliyokuwa imembeba Katibu Mkuu wa Chadema Dr. Wilbroad Slaa ikitua katika Uwanja wa Furahisha ili aweze kuhutubia katika Mkutano wa Kampeni wa Chadema M4C Pamoja Daima.
 Katibu Mkuu wa Chadema Dr Wilbroad Slaa akiingia Uwanjani ili aweze kuhutubia maelfu wa Wana Mwanza waliofika Kumsikiliza.
 Mbunnge wa Musoma mjini Vincent Nyerere akihutubia katika Mkutano wa hitimisho wa M4C Pamoja Daima leo katika viwanja vya Furahisha Jijini Mwanza.
 Mbunge wa Jimbo la Ilemela Highness Kiwia akitoa ya moyoni katika Mkutano wa Movement For Change Pamoja Daima.
 Mheshimiwa Higness Kiwia akimpokea Bwana Darius Ngoko ambaye ameamua kuhama chama cha Mapinduzi CCM na Kujiunga na Chadema katika Mkutano wa M4C Pamoja Daima.
 Katika hali ya kushangaza jeneza ambalo lilikuwa limechorwa picha ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zitto Kabwe nalo lilionekana mbele ya Kamera ya www.matukiomedia.blogspot.com kama inavyoonekana.
 Bwana Kaswahili aliyevaa shati la blue kamanda kutoka chama cha Chadema ambae anajiandaa kugombea katika Jimbo la Buchosa wilayani Sengerema akiangalia matukio yanayoendelea katika Mkutano huo.
 Mtumishi wa Mungu Mchungaji Amos Hulilo wa kanisa la Fpct Mjini Kati mwenye suti ya Blue akiwa amekaa Hightable akisikiliza hotuba mbalimbali katika uwanja wa Furahisha kwenye Kampeni ya M4C Pamoja Daima.
 Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Ilemela Bwana Laban Aggrey naee akiangali kwa umakini matukio kadha wa kadha katika steji wakati Mkutano wa M4C Pamoja Daima akiwa na baadhi Makamanda wa Chadema.
 Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasiana Maendeleo Chadema Bwana Wilfred Mganyizi Lwakatare akitoa speecha yake ya kusalimia Mkutano wa M4C Pamoja Daima katika viwanja vya Furahisha.
 Mdhamini wa Chadema Mzee Masinde akiongea kwa katika Mkutano wa M4C Pamoja Daima katika viwanja vya Furahisha.
 Mbunge wa Nyamagana Mheshimiwa Ezekia Wenje akiwa na Matibu wa Chadema Taifa Bwan Mudi mwenye kombati ya Green na Mbungue wa Jimbo la Ilemela Mheshimiwa Highness Kiwia.
 Nyomi ya watu wakiwa wamekaa wakisikiliza hotuba kutoka kwa Dr. Wilbroad Slaa kama inavyoonekana katika picha.
 Ze nyomiziiiiiii ndani ya uwanjaa wa Furahishaaa wakisikiliza hotuba mbalimbali kutoka kwa viongozi wa Chadema walioko kwenye Kampeni ya M4C Pamoja Daimaa.
 Katibu wa Chadema Taifa Dr. Wilbroad Slaaa akihuthubia maelfu ya watanzania waliofurika katika uwanja wa Furahisha Mwanza kusikiliza hitimisho la Kampuni ya M4C Pamoja Daima.

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kimesema hakitalalamika tena kwa lolote au kukilamu Chama Cha Mapinduzi CCM maana wameshaongea sana na sasa watafanya utekelezaji wa Ilani ya Chama chao.

Hayo yamesemwa na Katibu wa Chama hicho Dr. Wilbroad Slaa katika hitimisho la Kampeni za M4C Pamoja Daima lililofanyika katika uwanja wa Furahisha Mwanza.

Slaa amesema kuwa wameshaongea kero mbalimbali za wanainchi wa Tanzania lakini mpaka sasa hakuna kilichofanyika hicho wao kuanzia sasa waoa kama Chadema hawatalalamika zaidi ya kuchukua maamuzi ya utekelezaji tu.

Kampeni hizo ambazo imefanyika kwa siku 14 kwa kutembelea Majimbo yote ya upigaji kura ambazo zilikua zimegawanyika katika makundi mawili kwa kutumia chopa tatu ambazo zilikuwa zinaongozwa na Dr. Wilbroad Slaa, Freeman Mbowe na Tundu Lissu.

Tupe maoni yako