banner

.

.

Wednesday, 26 February 2014

MBUNGE WA MBEYA MHE JOSEPH MBILINYI A.K.A SUGU ASEMA MBEYA IMETULIA KUTOKANA NA UTENDAJI WAKE THABITI.


sugu_ea66c.png

Mbeya. Jimbo la Uchaguzi Mbeya Mjini linafahamika kwa rekodi yake ya kipekee.
Kwa muda mrefu lina rekodi ya kubadili wabunge kila baada ya miaka mitano. Hiyo imetokea kwa wabunge kama Polisya Mwaiseje (NCCR- Mageuzi), Benson Mpesya (CCM), miongoni mwa wengi.
Kwa sasa linashikiliwa na Joseph Mbilinyi 'Mr ll' au Sugu kutoka Chama cha Maendeleo na Demokrasia (Chadema )
.
Mr ll au Sugu ambaye kiumri ana miaka 42 aliupata ubunge huo kwa mara ya kwanza katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 2010.
Mbunge huyo ambaye pia ni msanii anaeleza mbinu alizofanya kulipata jimbo hilo, alichoahidi wakati wa uchaguzi, alivyotekelekeza na vikwazo anavyopata akiwa mbunge wa Mbeya Mjini, halmashauri ambayo inaongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
"Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka 2010, Chadema kupitia mimi katika Jimbo la Mbeya tuliahidi kurudisha madaraka kwa wananchi.

Tupe maoni yako