![]() |
William Zelothe Stepehen akiwa ndani ya ndege aina ya Airbus A319.
|

William
anafananisha anavyojihisi anapoiongoza ndege ya Airbus A319, na wakati
akiwa katika nyumba nzuri ya kifahari na ya kisasa; anaielezea ndege ya
Airbus A319 kama ndege iliyo imara na ambayo imewekewa mifumo mingi ya
usalama. Kwa maneno yake mwenyewe, anasema “Ndege ya Airbus inakulinda
kweli kweli, kama unaifahamu vyema”
William
amewahi kusomea usimamizi wa wanyama pori; alipata mafunzo ya urubani
kwa mara ya kwanza kule Florida Aviation Academy nchini Marekani mwaka
2006 ambapo alipata leseni yake ya usafirishaji kwa ndege. Ingawa ana
umri mdogo, ana uzoefu wa masaa 3,053 ya kuongoza ndege.
Kumwajiri rubani huyu mtanzania mwenye miaka 28, ni mojawapo ya jitihada za fastjet za kuhakikisha kuwa kampuni hiyo inaajiri watendaji wazawa waliobobea katika fani hiyo hapa nchini. Mikakati yao ya kuajiri pia ni mojawapo ya wajibu wao mpana wa kuwekeza nchini Tanzania. Kwa kila rubani aliyepokea mafunzo, fastjet imetumia gharama inayokadiriwa shilingi 49,546,400 hela za kitanzania ambayo ni sawa na 31,027 dola za kimarekani.
Tupe maoni yako

