banner

.

.

Wednesday, 22 January 2014

MAKALA: MFAHAMU COOLWIZZILA KATULA NDIMMILA JR CHIPUKIZI WA KANDANDA ANAYELIA NA URASIMU KATIKA SOKA NA KUKOSEKANA KWA SHULE ZA MICHEZO[ ACADEMY}



Na: JACKTAN MSAFIRI
 Mwanza.
Ni kijana mwenye umri wa miaka 17 mwenye kipaji cha hali ya juu katika kusakata kandanda ambaye anadai urasimu uliokithili wa viongozi katika kabumbu ndio chanzo cha kupoteza vipaji vya vijana

Akizungmza na mtandao wa   www.matukiomedia.blogspot.com
 hii katula amesema viongozi wenye dhamana sio ngazi kubwa hadi ndogo wamekuwa wenye kujinufaisha wao na vizazi vyao huku ubaguzi na upendeleo ukitawala katika club mbalimbali navyama vya soka hasa wilayani.

“Mimi nimeshiriki katika ligi mbalimbali za vijana ikiwemo kopa cocacola lakini ilifika sehemu nikaachwa kwa kuwa sikuwa na laki moja ya kutoa ili nijumuishwe katika ngazi ya taifa na walioweza kutoa waliendelea, kweli mkono mtupu haulambwi” alisema katula

Kijana huyo amesema kuwa kitu kingine kinachoporomosha soka la vijana ni kukosekana kwa shule za kuibua vipaji yaani academy,kukosekana kwa vifaa vya michezo na viwanja na uhaba wa ligi za vijana

Anasema “mimi ningekuwa raisi wa tff ningeanza kwa kurekebisha ligi kuu kwa kuongeza idadi ya timu angalau zifike 18 ili kuongeza ushindani na ningeongeza idadi ya ligi bila kusahau kuwekeza kwa hali ya juu katika soka la vijana”
Coolwizzila katula ndimmila(17)amezaliwa mjini nansio wilayani ukerewe katika mkoa wa mwanza,klabu alizowahi kuchezea ni nansio utd,kagera fc na muungano fc zote za wilayani ukerewe
Nafasi anazocheza uwanjani ni kiungo mshambuliaji na winga na jumla ya mechi rasmi alizocheza ni 109 akifunga magoli 65 ambapo malengo yake ni kucheza mpira wa kulipwa hasa nchini uingereza ambapo amesema anafanya kila liwezekanalo kuhakikisha anafanikisha malengo yake.

Alipo ulizwa kwa nini amechagua kandanda kati ya michezo yote amesema “mbali na kuwa na kipaji mchezo huu upo kwenye damu,na nimewahi kulala mtaani vibalazani baada ya kukosa mwenyeji nilipoenda kucheza fainali ya kombe la mbuzi katika wilaya ya kwimba ila sikuumia kwa kuwa nilijua najenga ndoto zangu na nilifunga magoli 3 peke yangu ambayo yaliipa ushindi timu yangu”

Mchezaji anayemkubali kwa hapa Tanzania ni  mlisho ngassa na ulaya anamkubali sana  Didier drogba.Katula amewaomba watu wenye uwezo wa kuendeleza ndoto zake wajitokeze kufanya hivyo kwa kuwasiliana na uongozi wa safu hii au kwa simu yake ya mkononi 0762646746

Tupe maoni yako