banner

.

.

Tuesday, 21 January 2014

FIRST LADY WA TANZANIA MAMA KIKWETE ASISITIZA KUPUNGUZA MAAMBUKIZI KUTOKA KWA MAMA KWENDA KWA MTOTO.

img_0858_04a5f.jpg

Na Magreth Kinabo – Maelezo

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amewataka Watanzania kuongeza juhudi za kuzuia maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi(VVU) kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto ili katika Tanzania iweze kuwa na kizazi kisichokuwa na VVU na ugonjwa wa Ukimwi.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) wakati akifungua mkutano wa kitaifa wa wadau wa kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

Aidha mama Kikwete aliwataka Watanzania kuchangia sh. 100 katika kupambana na tatizo kwa mchango utawapa nguvu wadau wengine kuwaunga mkono.

Aliwataka wadau wamaendeleo kuendele kuunga mkno katika juhudi za kuondokana na tatizo hilo.
" Lazima juhudi za makusudi zifanyike bila kuchoka kwa maeneo yote Serikali, NGO's, taasisi za dini mashirika ya kiraia na watu binafsi . Hii itasaidia kunusuru kizazi chetu na kuwa na nguvu kazi iliyobora, kizazi kisichokuwa na maambukizi na VVU na Ukimwi," alisema Mama Kikwete huku akisisitiza Tanzania bila Ukimwi inawezekana.
 
Aliongeza kuwa mikakati imara na endelevu ni lazima iwepo kama vile kutoa huduma za kuzuia maambukizi ya VVU na Ukimwi kwa kushirikisha jamii na kutoa tiba kikamilifu zinaweza kupunguza maambukizi hayo

Tupe maoni yako