banner

.

.

Saturday, 25 January 2014

ETOILE DU SAHEL wamruhusu Okwi Yanga: Waondoa jina lake CAF


JAMBO ambalo linaiumiza kichwa Yanga sasa ni kutaka kuhakiki kama kweli Etoile du Sahel imewasilisha jina la straika, Emmanuel Okwi kwenye usajili wake kwa Shirikisho la Soka Afrika (CAF).
Lakini katika orodha ya Etoile du Sahel, ambayo Mwanaspoti imepata nakala yake jana Ijumaa ni kwamba 

klabu hiyo imepeleka CAF majina 24 tu, na hakuna jina la Emmanuel Okwi.
Iwapo ikitinga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Etoile inaweza kuongeza majina sita kwani kila klabu inaruhusiwa kutuma majina 30.

Kwa kifupi ni kwamba, Etoile du Sahel haiwezi kumtumia Okwi katika Ligi ya Mabingwa Afrika na sasa Yanga wanaweza kumtumia raia huyo wa Uganda kwani wametuma jina lake katika shirikisho hilo mjini Cairo, Misri.

Etoile kwenye usajili wake wa CAF imepeleka wachezaji 24 ambao pia hakuna jina la Okwi.
Waliosajiliwa CAF ni Aymen Mathlouthi, Saif Ghezal, Ghazi Abderrazzak, Radhouene Felhi, Marouene Tej, Hamza Lahmar, Alaya Brigui, Baghdad Bounedjah, Abdel Fadel Suanon, Issam Jebali, Franck Kom, Ahmed Mortadha na Ben Ouannes

Tupe maoni yako