banner

.

.

Saturday, 4 January 2014

KWANEEMA FM RADIO YATOA TUZO KWA WAFANYAKAZI WALIOFANYA VIZURI 2013.

 Hapa Mkurugenzi wa Kwaneema Fm,akitoa maelezo juu ya Ufanisi wa kazi kwa wafanyakazi.


                Hapa ni Meneja wa kituo hicho Marium Juma,akitoa maelezo juu ya Tuzo..


                         Wafanya kazi wa kwaneema Fm,wakifuatilia tukio zima.


                Frola Jackson,ambae amechukua tuzo ya mfanya kazi bora wa usafi wa 98.2.


                  Mkurugezi Dinnah Mpemba katika Pozi safiiiiiiiiiiiiii sanaaaaaaaaaaaaa..........


                             Joshua Dede,akichekelea baada ya kupokea Tuzo............


                Erasto Juma akionesha cheti cha mbunifu bora katika kipindi cha kijana
 The Super Brand Joely Maduka,akipokea tuzo ya mtangazaji anayeongoza kwa kuleta wageni studio kwenye kipindi cha mazingira.

                     Maduka akichukua Picha ya Pamoja na Mkurugenzi wa Kwaneema fm.


                                      Ilikuwa ni Furaha na nderemo isiyo kifani....


Afisa Utawala Msaidizi ambaye pia ni Meneja Vipindi wa Kwaneema Fm Jackline Raphaely akionyesha cheti cha Mfanyakazi bora 2013 alichokipata leo baada ya kuibuka msomaji wa taarifa ya habari bora.


 Mzee wa Habariiiiiiiiiiiii, Chief Editor Jeston Kihwelu akipokea barua ya utambuzi kwa kazi yake.
                Captain Joshua Dede Mzee wa Kuntura akiangalia cheti chake kwa umakini.


     Erasto Juma na Joshua Dede wakiwa na Mkurugenzi wa Kwaneema Fm Dinnah Mpemba.


         
                    Picha ya jopo la Wafanyakazi na Watangazaji wa Kwaneema fm.


Washindi wa tuzo mbalimbali upande wa wanawake wakionekana mbele ya ofisi ya Kwaneema fm.


Mshindi wa Tuzo ya Mfanyakazi bora 2013 Jackline Raphaely akiongea juu ya  tuzo aliyopata kutoka kituo cha Redio Kwaneema fm.


                                             Jacktan Msafiri akiongea na Erasto Juma.


 
Mwandishi wa habari wa Kwaneema Fm Jacktan Msafiri akiongea na Joel Maduka juu ya tuzo aliyopata.


Fabian Fanuel C.E.O wa Matukio Media Blog akiwa na Meneja Msaidizi wa Kwaneema Fm Mariam Juma mbele ya Kamera.
Mmiliki wa Matukio Media Blog Fabian Fanuel akiwa na Mtangazaji wa Kwaneema Fm Joel Maduka.
Mhariri Mkuu wa Kwaneeema Fm Bw.Jeston Kiwelu na Maneja Msaidizi Mariam Juma wakishow mbele ya Kamera ya Matukio Media Blog.


Joel Maduka
Mwanza.

Imebainika kuwa kufanya kazi kwa wito pasipo kuweka Maslahi mbele ni silaha ya kushinda hali ngumu ya maisha.

Hayo yameelezwa na mkurugenzi wa kituo cha radio ya kwaneema Pastor Dinnar Mpemba katika hafla za kutunuku tuzo kwa wafanyakazi bora katika Mwaka wa 2013

Akiwataja washindi wa tuzo mbalimbali Meneja wa Kituo hicho Mariam Juma amewapongeza na kuwataka  wazidishe bidii katika kazi na kuzidisha ubunifu mwaka huu.

Kwa upande wao baadhi washindi wa tuzo hizo Joel Maduka, Spencioza Haule, Frola John wameelezea hisia zao baada ya kupata tuzo na kuahidi kujituma zaidi kwa mwaka huu mpya ambao anaanza.

Naye Meneja wa vipindi katika kituo hicho Jackline Raphael ambaye ndiye Mshindi wa tuzo ya Mfanyakazi bora ameeleza Siri ya Ushindi wake kuwa ni Mungu na pia kujituma sana katika kazi bila kijihurumia.

Tuzo zilizotolewa ni katika ngazi ya Mfanyakazi bora wa Mwaka mbunifu,Mfanya shughuli kwa kujituma,Mfanyakazi anayejitolea katika kazi ka ziada Mtunza muda na aliyefanya vizuri katika kuleta wageni katika vipindi.



Tupe maoni yako