banner

.

.

Saturday, 8 March 2014

MAMA SALMA KIKWETE AZINDUA KAMPENI YA UCHUNGUZI WA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI NA SARATANI YA MATITI KATIKA SIKUKUU YA WANAWAKE DUNIANI JIJINI MWANZA.













Joel Maduka
Mwanza

UCHUNGUZI wa saratani ya mlango wa kizazi na saratani ya matiti umezinduliwa leo mkoani mwanza kwa katika kuadhimisha siku ya mwanamke duniani.

Akizindua uchunguzi huo  Mwenyekiti wa Wama Mama Salma Kikwete,amesema kuwa ni vyema kwa wadau wa maendeleo, kuhakikisha kuwa wanatoa elimu kwa wanawake kwani  unapo muelemisha mwanamke mmoja ni sawa umeelimisha watu wengi katika jamii.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Serikali Dk,Deonard Mbando,amesema kuwa Tanzania ni nchi ambayo imekuwa na kiwango kikubwa kwa tatizo la saratani ya kizazi.

Aidha Mwenyekiti wa Madaktari Wanawake Tanzania,Dk Serafina Mkuwa,ameongeza kuwa  saratani ya mlango wa kizazi ndio inaongoza kwa kuwapata wanawake wengi na kusababisha vifo vingi hasa katika nchi zetu za kiafrika ikiwemo Tanzania.

Uzinduzi wa saratani ya kizazi na saratani ya matiti umezinduliwa leo katika viwanja vya Nyamagana jijini Mwanza,huki ikiwa imebeba kauli mbiu isemayo tuungane pamoja katika kutokomeza  saratani ya mlango wa kizazi Tanzania, nani kama Mama.




Tupe maoni yako