
"Ni vyema tukatambua kuwa Watanzania ni wapenda amani, hivyo wasingependa kuona kukijitokeza tofauti kati ya wajumbe wa Bunge hilo.
Dar es Salaam. Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Kardinal Pengo amesema shughuli za mchakato wa Katiba zifanyike kwa amani na kwamba ziwalinde Watanzania katika umoja na mshikamano waliyokuwa nao.
Pia, amewataka wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kuweka masilahi yao kando na kutanguliza masilahi ya taifa kwa faida ya Watanzania.
Tupe maoni yako
