Na Mwandishi Maalum, New York
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imesema, posho ya dola 1.28 kwa siku wanayolipwa walinzi wa amani wanaohudumu katika Misheni za kulinda amani za Umoja wa Mataifa, hailingani na mazingira magumu na hatari ya utekelezaji wa mamlaka wanayokabidhiwa na Umoja wa Mataifa.
Na kwa sababu hiyo ,na kwa zingatia hali halisi, Tanzania imesisiza kwamba, wakati umefika sasa wa kuangalia upya posho hiyo ambayo imedumu kwa zaidi ya miaka 20.
Balozi Tuvako Manongi, Muwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa mataifa, ametoa rai hiyo mwanzo mwa mkutano wa Kamati Maalum ya Usimamizi wa Operesheni za Ulinzi wa Amani maarufu kama C-34.
Kamati hii ambayo wajumbe wake ni kutoka nchi zinazochangia walinzi wa Amani katika misheni mbalimbali za kulinda amani, imeanza mkutano wake wa mwezi mmoja hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa ambapo wajumbe watajadili mambo yote yanayohusu sera za ulinzi wa Amani chini ya Umoja wa Mataifa.
Balozi Manongi amewaeleza wajumbe wa mkutano huo kwamba Kamati ilikuwa inaanza mkutano wake, wakati ambapo , operesheni za ulinzi wa amani zinakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwamo za malipo duni.
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imesema, posho ya dola 1.28 kwa siku wanayolipwa walinzi wa amani wanaohudumu katika Misheni za kulinda amani za Umoja wa Mataifa, hailingani na mazingira magumu na hatari ya utekelezaji wa mamlaka wanayokabidhiwa na Umoja wa Mataifa.
Na kwa sababu hiyo ,na kwa zingatia hali halisi, Tanzania imesisiza kwamba, wakati umefika sasa wa kuangalia upya posho hiyo ambayo imedumu kwa zaidi ya miaka 20.
Balozi Tuvako Manongi, Muwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa mataifa, ametoa rai hiyo mwanzo mwa mkutano wa Kamati Maalum ya Usimamizi wa Operesheni za Ulinzi wa Amani maarufu kama C-34.
Kamati hii ambayo wajumbe wake ni kutoka nchi zinazochangia walinzi wa Amani katika misheni mbalimbali za kulinda amani, imeanza mkutano wake wa mwezi mmoja hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa ambapo wajumbe watajadili mambo yote yanayohusu sera za ulinzi wa Amani chini ya Umoja wa Mataifa.
Balozi Manongi amewaeleza wajumbe wa mkutano huo kwamba Kamati ilikuwa inaanza mkutano wake, wakati ambapo , operesheni za ulinzi wa amani zinakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwamo za malipo duni.
Tupe maoni yako