banner

.

.

Friday, 28 February 2014

MAAFISA Afya na Mifugo wametakiwa kutobweteka maofisini na kufanyia kazi kwenye makaratasi(Paper Work) badala yake wafanye kazi kwa vitendo



Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya, Dk. Agnes Buchwa, alipokuwa akifungua kikao cha watendaji wa Halmashauri za Wilaya na Jiji la Mbeya kuhusu Shughuli za Mamlaka ya Udhibiti wa Chakula, Dawa, Vipodozi na Vifaa tiba(TFDA) kilichofanyika katika ukumbi wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya uliopo Forest Mpya Jijini hapa.

Kaimu Meneja wa Mamlaka ya udhibiti wa Chakula, Dawa, vipodozi na vifaa tiba(TFDA) Kanda ya Nyanda za juu Kusini, Rodney Alananga,ambao ndiyo wandaaji wa mafunzo hayo alisema yamewalenga Maafisa afya, Mifugo, Famasia na wahasibu kutoka Halmashauri za Wilaya na Jiji la Mbeya.


MAAFISA Afya na Mifugo wakiwa katika semina hiyo




Picha ya pamoja
MAAFISA Afya na Mifugo wametakiwa kutobweteka maofisini na kufanyia kazi kwenye makaratasi(Paper Work) badala yake watumie taaluma yao kama walivyofundishwa mashuleni kwa kufanya kazi ya vitendo.
Mwito huo umetolewa na Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya, Dk. Agnes Buchwa, alipokuwa akifungua kikao cha watendaji wa Halmashauri za Wilaya na Jiji la Mbeya kuhusu Shughuli za Mamlaka ya Udhibiti wa Chakula, Dawa, Vipodozi na Vifaa tiba(TFDA) kilichofanyika  katika ukumbi wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya uliopo Forest Mpya Jijini hapa.

Tupe maoni yako