Na Peter Fabian
MWANZA.
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Mbaraka Abduwakili amewataka wajumbe wa Baraza kuu la Taifa Idara ya Uhamiaji nchini kujikita zaidi kujadili utendaji kazi wa watumishi wa Idara hiyo.
Kufanya thathimini ya utendaji wa watumishi ambao baadhi yao wamekaa muda mrefu kwenye vituo vyao vya kazi na kuzoeana hali ambayo imedaiwa na kudhaniwa kuwa inazorotesha ufanisi wa majukumu ya kila siku na hata huduma kutolewa kwa wageni na wananchi bila kukidhi ubora wa maadili ya viapo vya kazi.
Kufanya thathimini ya utendaji wa watumishi ambao baadhi yao wamekaa muda mrefu kwenye vituo vyao vya kazi na kuzoeana hali ambayo imedaiwa na kudhaniwa kuwa inazorotesha ufanisi wa majukumu ya kila siku na hata huduma kutolewa kwa wageni na wananchi bila kukidhi ubora wa maadili ya viapo vya kazi.
Akifungua Mkutano mkuu wa
Baraza hilo jana Jijini Mwanza , alisema kwamba baadhi ya askari na
watumishi wa Wizara yake wanadaiwa kukaa muda mrefu sehemu moja ikiwa ni
kwenye vituyo vyao vya kazi jambo ambalo linachangia baadhi yao
kushindwa kutekeleza majukumu yao na kujihusisha na ulevi na vitendo
ambavyo haviruhusiwi na kuzorotesha ufanisi wakati wa utowaji huduma.
Abduwakili alisema kwamba
mazoea ya watumishi hao wa Idara zilizo chini ya Wizara yake ni vyema
wakazingatia viapo vya utendaji wao wa kazi na kujikita kutoa huduma kwa
ufanisi zaidi kwani hata solidalite yao inasema kwamba masilai bora
kwanza lakini pia utendaji bora wa kazi.
Abduwakili aliwataka
wajumbe 130 ambao ni wawakirishi wa watumishi na viongozi wa vyama vya
wafanyakazi katika Idara za Uhamiaji kutoka Mikoa yote nchini
kuzingatia kujadili uboreshwaji wa utendaji kazi zaidi pamoja na kuweka
mapendekezo ya kuboreshewa masilahi yao lakini wawafikishie ujumbe wa
kufanya kazi kwa ufanisi zaidi kwenye vituo vyao vya kazi.
Tupe maoni yako
