banner

.

.

Tuesday, 1 April 2014

PASAKA GOSPEL FESTIVAL 2014 YAJA KA KISHINDO NDANI YA CCM KIRUMBA MWANZA.


Joel Maduka
Mwanza
Wakazi wa Mikoa yote ya Kanda ya Ziwa wameombwa kujitokeza kushuhudia tamasha kubwa la Muziki wa Injili linalojulikana kama Pasaka Gospel Festival 2014 ambalo linaandaliwa na Kampuni ya The Great Zone Entertainment katika Sikukuu ya Pasaka Mwaka huu katika Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza .

Haya yamesemwa na Mratibu wa Tamasha hilo bwana  Fabian Fanuel wakati akizungumza na waandishi wa habari wakati akizungumzia ujio  mkubwa wa Tamasha hilo katika msimu huu wa sikukuu za Pasaka za mwaka huu jijini Mwanza.

Fanuel amesema kuwa tamasha la Mwaka huu lina  utofauti mkubwa na la Mwaka jana maana maandalizi ya Mwaka huu yako vizuri  na pia yameanza mapema ili kuhakikisha  wanatoa burudani ambayo kila mtu atakayefika uwanjani hapo ataifurahia, katika kumbukumbu ya  kufufuka Mwokozi Yesu  Kristo.

Amesema tamasha la mwaka huu litafanyika kwa siku mbili mfululizo katika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza tarehe ishirini mwezi wa nne na tarehe ishirini na moja mwezi wa nne mwaka huu ambalo  litakuwa tofauti sana na miaka yote iliopita maana lenyewe litakuwa la siku mbili.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya The Great Zone Enteratainment Bi. Masele Malekela amesema kuwa tamasha la mwaka huu litakuwa kubwa sana kutokana na mialiko ya waimbaji wakubwa na wakipekee wa Muziki wa Injili  ambao hawajawi kufanya huduma  Mwanza. 

“Mwaka huwa tumejipanga vizuri sana  kwa maandalizi makubwa  ili kuwapa watazamaji na mashabiki  wa matamasha yetu, tamasha kubwa na lenye ubora na kiwango cha juu kitaifa”

Amewataja waimbaji kutoka Dar es salaam kuwa ni Beatrice William wa BSS, Sheikh Jamal Jojo, Lusekelo Samwel, Chamwenyewe Jembe, Jessica Julius, na kutoka Nzega Seiri Andrew, Kutoka Shinyanga Sarah Abel, na Kutoka Mwanza Christina Victor, Rebeka Pius, Paulo Shole, Ajuaye Onesmo, Caphlen Joseph.

Katika tamasha hilo la jumapili ya Pasaka kuna uzinduzi wa Filamu mpya ya kikristo uitwayo Rafael ambayo imeigiziwa katika jiji la Mwanza, pia siku hiyo kutakuwepo waimbaji wakali wa Muziki wa Injili kusindikiza uzinduzi huo. Jumatatu ya Pasaka kuna mashindano ya kwaya ili kupata mshindi wa kwanza ambaye atajinyakulia zawadi nzuri ili kumtia motisha katika kazi ya uinjilishaji.

Tupe maoni yako