banner

.

.

Monday, 8 May 2017

K.K.K.T DAYOSISI YA MASHARIKI YA ZIWA VICTORIA USHARIKA WA YERUSALEM MABATINI MWANZA. HISTORIA YA KWAYA YA NEEMA.



                     HISTORIA YA KANISA KWA UFUPI    
Kanisa la K.k.k.t Yerusalemu mabatini Mwanza lilianza mwaka 1960 likiwa chini ya Mwinjilisti Ella Pyuza ambaye kwa sasa ni marehemu,kwa wakati huo walikuwa wakiabudia katika majengo ya Laini polisi Mabatini Mwanza.Baada ya muda kupita walihama pale walipokuwa wakiabudia na kuelekea katika Shule ya Msingi ya Pamba Primaly school iliyopo Mabatini Mwanza hapo ndio wakawa wakiabudia wakiwa chini ya Mwinjilisti Mwakalasia na baada ya muda kupita walipata kiwanja kilichopo maeneo ya Mabatini Mwanza na wakaanza ujenzi wa kanisa huku wakishirikiana na waumini pamoja na mafundi na mwaka 1996 walianza kusali katika kanisa walilolijenga na kwa wakati huo ulikuwa ni Mtaa wa Yerusalemu Mabatini ukiwa chini ya Mwinjilisti Pendaeli Ulio, na baada ya muda kupita wakapata nafasi yakuwa Ushalika wa Yerusalemu Mabatini huku ukiwa chini ya Mwinjilisti William Msokwa.  

 MAFANIKIO YA KANISA KWA UFUPI          
Kanisa la Yerusalemu mabatini Mwanza K.k.k.t limeweza kufanikiwa kufungua kanisa lingine ambalo lipo mtaa wa Mahina Mwanza ambapo kanisa ilo linatambulika kwajina la Mtaa wa Bethania Mahina K.k.k.t,pia Ushalika wa Yerusalemu Mabatini umefanikiwa kuweka vigae ndani yakanisa,pamoja na mengine mengi.
         
HISTORIA YA KWAYA YA NEEMA/KUANZA KWAKE.
Kwaya ya Neema ilianzishwa mwaka 1997 ikiwa chini ya Mwenyekiti Aliko Ibrahim, ikiwa na waimbaji kumi na tatu (13) chini ya mwalimu Jacobo Mwaikibaya, wakati huo wakiimba kwa kutumia vyombo vya asili kama vile Ngoma, Filimbi, Chupa za Soda n.k, Neema kwaya ilianza na waimbaji kumi na tatu (13) ambao kwa majina yao ni; Boniphace Mwandunga, Jacobo Mwaikibaya, Ibrahim Aliko, Emmanuel Nkombe, Samwel Marick, stella Fredy Mwasilembo, scolastika Fredy Mwasilembo, Nuru Makea Mwambemba, Dorah Makea Mwambemba, Aliko Wanki, Richard Robert, Esther Robert, Mr’s Tito, Pia kwa wakati huo kwaya ilikuwa na mlezi mmoja ambaye ni Mzee Mwambemba ambaye kwa sasa ni Marehemu.

MABADILIKO YA UONGOZI.
Kwaya ya Neema tuliamua kufanya uchaguzi wa viongozi wa kwaya mnamo mwaka 2004, kwa kuanza na ngazi ya Mwenyekiti tulimchagua ndugu Jacobo Mwaikibaya kama Mwenyekiti mkuu wa kwaya na Msaidizi wake alikuwa ni Andrea Andrew, huku katibu alikuwa ni ndugu Mr Francis na katibu msaidizi alikuwa ni Edward Somi. Pia mnamo mwaka 2007 kwaya ilifanya uchaguzi mwingine wa viongozi baada ya kuwa uongozi uliopita muda wake kuwa umeisha na wengine kuhama, ambapo mwenyekiti tulimchagua ndugu Colnel Siyola, msaidizi wake  akiwa Loyce Andrea na katibu tulimchagua ndugu Edward Somi na msaidiizi wake akiwa ni Frola Daudi ambaye pia ndiye Mwalimu wa kikundi, pia kwaya ilimchagua ndugu Nickson Petro kuwa mtunza hazina wa kwaya. Kwaya ya Neema iliamua pia kufanya uchaguzi wa walezi ambao kwa majina yao ni; Loyce Maulilo, Samwel Marick, Blanka Ngoi na Anneth Limo, pia kwaya ilimchagua M’rs Eliyawinga Mungule kuwa Mshauri wa kwaya.
MAFANIKIO
Kwaya ya Neema tulifanikiwa kununua vyombo vya muziki vya kisasa kwa kuchangishana wanakwaya na zingine kuchangiwa na kanisa na tukaweza kununua, Kinanda PSR 1100, Speaker mid mbili (2), na Stendi za Speaker mbili (2).

Mnamo tarehe 17/11/2009 kwaya ya Neema tulifanikiwa kurekodi Albam ya kwanza ambayo ni Audio iitwayo MOTO WA JEHANAM tuliyoirekodia katika Studio ya Habari Maalum. Na ilipofika mwaka 2010 kwaya ya Neema tulizindua Albam hiyo iliyofahamika kwa jina la MOTO WA JEHANAM Katika viwanja vya kanisa la K.K.K.T Mabatini Mwanza.

Pia ilipofika mwaka 2011 kwaya ya Neema tulirekodi Audio ya pili na kutoa mkanda wa Video katika studio ya One Love Studio. Na mnamo mwaka 2015 kwaya ya Neema tulifanikiwa kuzindua albam hiyo katika viwanja vya kanisa la K.K.K.T Mabatini Mwanza. Pamoja na mafanikio hayo yote kwaya ya Neema kwa sasa tuna jumla ya waimbaji ishirini na tano (25) ambapo waimbaji wa kiume idadi yao ni waimbaji kumi na tano (15) na idadi ya waimbaji wa kike ni kumi (10).

 Na pia tunapenda kuwashukuru wale wote ambao walikuwa wakishirikiana nasi na bado wanaendelea kushirikiana nasi kwa kutupa michango yao ili kuhakikisha kikundi hiki kinapiga hatua, tunawashukuru viongozi na waumini wote wa Yerusalem Mabatini pamoja na watu binafsi bila kusahau Media zote ambazo zimekuwa zikitupa ushirikiano kwa kupiga nyimbo zetu hasa Redio kwa Neema fm bila kumsahau Fabian Fanuel kwa ushirikiano ambao anaendelea kuuonesha. Hivyo tunasema Mungu awabariki sana.
                                          
 CHANGAMOTO
Siku zote palipo na mafanikio huwa hapakosi changamoto, kwaya ya Neema tunazo changamoto nyingi sana katika huduma hii ambazo ni pamoja na;
(a) Ukosefu wa vyombo vya muziki hasa baada ya kuunguliwa na vyombo vyetu vyote (b) Ukosefu wa usafiri wa uhakika pindi kwaya inapokuwa na safari ya kupeleka injili sehemu mbalimbali (c) Ukosefu wa wataalam wa muziki, hivyo inakuwa inatulazimu kutoa pesa kwaajili ya kupigiwa muziki (d) Ukosefu wa walimu ambao ni watunzi wazuri wa nyimbo (e) Kwaya inaukosefu wa miradi na hivyo kutulazimu kuchangishana pesa wenyewe kwa wenyewe ili tuweze kupata kile tunachohitaji.

MALENGO YA KWAYA
Kwaya ya Neema tuna malengo mbalimbali ambayo ni kama ifuatavyo; (a) Kwaya ya Neema tuna malengo ya kununua vyombo vya muziki vya kisasa (b) Pia tunayo malengo ya kuanzisha miradi midogo midogo (c) Tuna malengo ya kurekodi audio na Video.


MIKAKATI YA KWAYA YA NEEMA/MALENGO TARAJIWA
 Kwaya ya Neema tunamikakati mingi sana ambayo Mungu akitupa Neema tungependa kuyakamilisha,mikakati hiyo nikama ifuatavyo,(a)Mungu akitupa neema tunatarajia kununua kiwanja cha kujenga maduka 5 yakukodisha, pamoja na shule ya awali ya chekechea.(b)Pia tunatarajia kununua costa 2 kwaajili ya biashara ili kwaya iweze kunufaika katika suala zima la kujikimu kifedha na kiuchumi.Yote haya tutayakamilisha pale ambapo tutapata neema ya kupata wafadhili wakutuwezesha ili yote yaweze kutimia.

MAHITAJI YETU KAMA KWAYA
Kwaya ya Neema tuna mahitaji mbalimbali ili tuweze kupiga hatua zaidi na mahitaji yenyewe ni kama ifuatavyo; (a) Tunahitaji kuwa na kompyuta ili tuweze kutunza kumbukumbu za kwaya kwa ufasaha zaidi. (b) Tunahitaji kuwa na GARI la usafiri litakalotuwezesha kutoa huduma au kupeleka Neno la Mungu sehemu mbalimbali kwa urahisi (c) Pia tunahitaji kupata wafadhiri ambao wataweza kutusaidia katika huduma hii ya uimbaji 

WITO KWA KWAYA
Tukiwa kama kwaya ya Neema tunatoa wito kwa kwaya zingine kuwa huduma hii ya umbaji ina changamoto nyingi sana, hivyo ni  muhimu kuwa na umoja mzuri pindi tunapokuwa na wanakwaya wetu. Pia tunatakiwa kuwa wavumilivu kwani kuna kukata tama na mwisho ni kikundi kuvurugika, ni muhimu sana kusimama katika maombi na kumsihi Mungu aweze kutuinua katika huduma hii, na ni vizuri tuwe na nidhamu kwa viongozi wetu wa makanisa na viongozi wa kwaya na tuweze kushirikiana na jamii vizuri ili waweze kumjua Mungu kwa kupitia nyimbo zetu.

Kuwapata unaweza kuwasiliana nao kwa mawasiliano yao kama ifuatavyo:
 Po box Number  11592.
Phone Number  0756-831375/0625-812573 Mwenyekiti.
                        0767-154418/0624-129297 Katibu.

Tupe maoni yako